
Kijarida 2009
Mama ni dhahabu aliyonitendea siwezi kuhesabu
Habari Kutoka Tanzania 2009
Trui Goslinga alikuwa Tanzania kuanzia tarehe 10 Februari mpaka tarehe 8 Machi kwa ajili ya kufanya tathmini ya miradi ya VICOBA. Nia yake ilikuwa kuvitembelea vikundi vinne vya VICOBA na pia kujaribu kupata utatuzi kuhusu uzio wa kiwanja cha Kalimata. Vifaa vyote vya uzio vimeisha nunuliwa ila kibali cha kujenga huo uzio kilikuwa hakijapatikana. Wiki ya mwisho kabla Trui hajaondoka kule Kalimata walipata kibali cha kuweka uzio. Kwa sasa kiwanja kimeisha zungushwa uzio.
Mfumo wa kuweka na kukopa (VICOBA)
Utaratibu huu unaendelea vizuri. Akina mama wa Kali Mata Gezaulole hukutana mara moja kila wiki na kila mmoja huweka hisa ya shilingi 6,000 (€ 3,50). Baada ya kila mtu kuweka hiki kiwango, kina mama huomba mkopo. Utaratibu ni kwamba mkopo huo usizidi mara tatu ya hisa iliyowekwa. Kina mama husaidiana kupanga makadirio ya miradi yao. Yeyote anayechelewa kwenye mkutano hutozwa faini ya shilingi 600. Akina mama wanaheshimu sheria za VICOBA na wanazitekeleza vizuri.
Kikundi cha pili cha VICOBA kilichoanzishwa ni cha Mama Lyimo, mwanachama wa ‘Support Group’ kinaitwa ‘The Kicheko Group’ kilichopo Msimbazi Centre Dar es Salaam. Kina mama huwasilisha maombi ya mikopo na kuidhinishwa. Baada ya hapo mikopo hutolewa. Ikibainika kuwa sheria hazifuatwi vizuri humwomba mkufunzi Ali Ismael ili atoe ushauri wake. Je mikopo hutumikaje? Huitumia kununulia kanga na vitenge na kuviuza, pia kuanzisha sehemu ya kushonea nguo. Hukausha samaki ili wawauze, huuza maji ya kunywa, mitumba, kuchakata magazeti ya zamani (ili kuyatumia tena kwa njia zingine) Pia huotesha mboga za majani kama mchicha, maharage na viazi vitamu.
Kikundi cha tatu cha VICOBA ni cha kanisa la (WAPO) World and Peace Organisation cha Mama Nguma (Support Group) Je akina hutumiaje mikopo yao? Akina mama hufanya biashara ya asali, kuku, rosella ambayo husaidia kushuka kiasi fulani cha mafuta yanayozidi mwilini. Mmoja wa akina mama ameanzisha chekechea yenye watoto wapatao 25. Huyu mama hutumia mkopo wake kununulia vifaa kwa ajili ya hii chekechea.
Kikundi cha nne cha VICOBA ni cha Umoja wa Makonga, ambao ni Wamakonde. Hawa wanaendesha biashara zao katika mitaa ya jiji la Dar-es-Salaam Kikundi hiki ni mchanganyiko, wa akina baba na akina mama. Kwa hali hiyo hushauriana kwanza kabla ya kubadilisha sheria.
Ali Ismael anaongoza hiki kikundi. Wanakikundi hawa hutumia mikopo yao kwa biashara zifuatazo: kuchakata magazeti ya zamani (ili kuyatumia tena kwa njia zingine) na kununulia mitumba. Wakati fulani mwanachama mmoja alipewa mkopo ambao aliweza kuulipa pamoja na riba kubwa.
Nyumba ya Kulala Wageni na Utalii.
Nyumba imefanyiwa marekebisho. Kuta zimepakwa rangi. Mikeka mipya imewekwa darini. Msanii Ndula amechora picha tatu za mandhari ya kijiji cha Gezaulole kwenye sehemu ya nje inayotumika kwa chakula na kupumzikia Unaweza kungalia pia tovuti ifuatayo. www.vrouwen.net/kalimata Mwaka huu Juliana amepokea wageni 62.
Kwa mara ya nne wageni kumi na mmoja wa Kikundi cha Utalii cha ‘Wederzijds’ walilala hapo siku moja. Walitembezwa kijijini Gezaulole na walikaribishwa kwa chakula kitamu nyumbani kwa akina mama.
Renee Duffhues ( mwanachuo anayechukua fani ya Lugha za Kiafrika Chuo Kikuu cha Leiden) alikaa wiki mbili Gezaulole kuboresha Kiswahili chake.
More pictures >
Mradi Wa Shule ya msingi ya Mboa Maji ulifanikiwa. Kwa kushirikiana na msanii Ndula watoto walichora picha nyingi na walicheza ngoma za jadi wakiongozwa na wanamuziki walioandamana na Ndula.
Nishati ya Nguvu za Jua
Watoto wa Hadya Mkendwa wamemzawadia mama yao na familia yake chombo kinachotoa mwanga kutokana na nishati ya nguvu za jua. Wenyeji wa Mboa Maji wapatao sita wameweka pia vyombo vinavyotoa mwanga wa nishati ya nguvu za Jua majumbami mwao.
Mkutano mkubwa unaohusu Mabadiliko ya Hali Ya hewa unategemewa kufanyika kwenye nyumba ya wageni Gezaulole Wageni 43 wanategemewa kuhudhuria huo mkutano. Watazungumzia kuhusu maji, moto, takataka za plastiki na vyanzo vya nishati. Watajadiliana kutokana na ujuzi walionao, watatengeneza mabango, mashairi na michezo ya kuigiza.
Habari kutoka Finland 2009
Uingizaji wa Henna.
Mwaka 2009 Tampere Fair Trade Shop (duka la soko nafuu Tampere) waliingiza vifurushi 1000 vya hina toka Kalimata Tanzania. Hina waliyoagiza kwa sasa iko njiani kutoka Tanzania.
Maduka kama ya Salon Mailis, mjini Jyväskylä na Hins IIkka, Toijala huwapaka nywele wateja wao kwa njia ya kitaalamu kwa kufuata masharti ya afya. Huwauzia pia hina wateja wao waweze kutumia nyumbani. Uuzaji wa hina pamoja na duka la vitu kutoka nchi zinazoendelea jijini Helsinki liitwalo “World in the “Village Activity” na “Market for Possibilities” ni muhimu sana Hameenlima na Turku.
Utalii
Chama Cha Usafiri wa Biashara Kinachoendeshwa kwa Maadili ya Haki Sawa na Kampuni ya Uwakala wa Usafiri ya Ms. Mari Mero Helsinki hushirikiana na Kalimata Finland. Wageni kadhaa toka kwenye haya mashirika hutembelea Kalimata Gezaulole.
Habari Kutoka Uholanzi 2009
Mipango ya 2010
Mural by Ndula, artist in Dar es Salaam
Tunatoa shukrani zetu kwa: Hilda Bestevaar (aliyefikisha miaka 80), Remonstrantse Gemeente Oosterbeek, NPB Bennekom, Soroptimisten Steunfonds Enschede, Prot. Gemeente Dokkum, na kwa wafadhili wote kwa misaada yao, na wote waliojitolea kusaidia katika shughuli mbali mbali za Kali Mata.
Kijarida hiki kinachapishwa kwa lugha ya Kiingereza, Kiholanzi na Kifinish.
January 2010
Nyumba ya wageni ya Kali Mata ina vyumba vitatu vya kulala, vitanda vitatu vya kienyeji na vyandarua na shuka za kutosha.Bei ya chumba chenye kitanda kimoja ni shilingi 5,000 na chumba chenye vitanda viwili ni shilingi 4,000 (€ 2,40) kila mmoja kwa usiku mmoja.
Wakati wa mchana unaweza kula sehemu zifuatazo:
• Kwenye nyumba ya wageni ya Kali Mata au nyumbani kwa akina mama 16 wa Kali Mata. Unaweza kupata msaada kwa Juliama kuhusu mpango wa kuweza kula kwa akina mama wa Kali Mata. Bei ya chakula mi shilingi 4,000 kwa mtu mmoja.au kwenye duka la Angela Mlowo au kwenye vihoteli vidogo vidogo vilivyoko kando kando ya barabara.
Usafiri kutoka Kigamboni hadi Gezaulole kwa dala dala ni shilingi 500 au kwa teksi shilingi 15,000. Uwe makini kuangalia ubao ulioandikwa KALIMATA GUESTHOUSE ambao umefungwa kwenye mti wa mwembe upande wa kulia.
Kwa habari zaidi wasiliana kwa simu zifuatazo:
• Elizabeth Malocho enmalocho@hotmail.de , GSM +255 (0) 784976984• Juliana Selestini, GSM + 255 782704716.